Muhtasari kuhusu Jimbo la Iringa na Parokia Zake.

Parokia ni jumuia rasmi ya waamini ambayo imeundwa kwa namna ya kudumu ndani ya Kanisa maalumu na imekabidhiwa kichungaji kwa paroko kama mchungaji wake chini ya mamlaka ya Askofu wa jimbo. Ni juu ya Askofu wa jimbo tu kuanzisha, kufuta na kubadilisha parokia.

Kanisa la Moyo Mtakatifu wa Yesu
Kanisa kuu la dayosisi hiyo lipo Iringa kilomita chache kutoka katikati ya jiji eneo la Kihesa.