|

Jimbo Katoliki la Iringa lapata mapadre wapya wanne (4) .

Daraja Takatifu la Upadrisho limetolewa na Mhashamu Baba Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa wa Jimbo  Katoliki la Iringa ambako ibada  imefanyika kwenye viwanja vya Kanisa Kuu la Kiaskofu la Moyo Mt. Wa Yesu Parokia ya Kihesa, siku ya Alhamisi tarehe 26, Agosti 2021.

Adimisho hilo lilitanguliwa na ibada ya masifu jioni ambapo mashemasi hao waliweka viapo siku ya Jumatano jioni.

Waliopata daraja hilo ni Shemasi Florence Ngerangera wa Parokia ya Usokami, Shemasi Gelasius Mwalongo- kutoka Parokia ya Ujewa, Shemasi Mathew Kilamlya wa Shirika la Bikira Maria Consolata kutoka Parokia ya Ilole na Shemasi Nelson Fungo kutoka Parokia ya Kaning’ombe. Katika homilia yake Mhashamu Baba Askofu Ngalalekumtwa amewataka mapadre hao wapya kuihubiri Injili kwa uaminifu, kulichunga Taifa la Mungu, kuongoza sio kwa kuonyesha mkono bali kwa mwenendo wao na kuziadhimisha Ibada Takatifu.

Pichani kutoka Kulia: Pd. Nelson Fungo , Pd. Mathew Kilamlya IMC, Pd. Florence Ngerangera, na Pd. Gelasius Mwalongo.

Maadhimisho hayo pia yameenda sambamba na sherehe za Yubilei ya miaka 25 ya Upadre, kwa mapadre wanne. Walioadhimisha Yubilei hiyo ni Padre Aidan Ulungi- Afisa Tawala Jimbo, Mkurugenzi wa Shirika la Kipapa la Utoto Mtakatifu Jimbo, pia ni mkurugenzi wa shule za Mt. Dominiko Savio zilizoko Jimboni Iringa, Padre John Mlomo Paroko wa Parokia ya Kilolo na Mkurugenzi wa Uchungaji Jimbo, Padre Romulo Mkongwa Paroko wa Parokia ya Mgololo na mlezi wa Radio Maria Jimbo Katoliki la Iringa, pamoja na Padre Joseph Magani kutoka Jimbo Katoliki la Lindi – mhadhiri wa Chuo kikuu cha Kikatoliki Ruaha ( RUCU)

Pichani kutoka Kulia: Pd. John Mlomo , Pd. Aidani Ulungi na Pd. Romlo Mkongwa.

Ibada ya maadhisho hayo yamehudhuriwa na mapadre zaidi ya 100 kutoka ndani na nje ya Jimbo la Iringa, watawa wa kike na kiume, pamoja na waamini walei kutoka ndani na nje ya Jimbo la Iringa.

Similar Posts

4 Comments

  1. There are actually a lot of particulars like that to take into consideration. That is a nice point to deliver up. I provide the ideas above as basic inspiration however clearly there are questions like the one you deliver up where crucial factor will be working in honest good faith. I don?t know if finest practices have emerged around things like that, however I’m positive that your job is clearly identified as a good game. Both girls and boys feel the impact of only a second’s pleasure, for the remainder of their lives.

  2. Unquestionably believe that which you said. Your favorite justification seemed to be on the web the simplest thing to be aware of. I say to you, I certainly get annoyed while people consider worries that they just do not know about. You managed to hit the nail upon the top and defined out the whole thing without having side effect , people can take a signal. Will likely be back to get more. Thanks

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *